Breaking News
Loading...
Tuesday, May 13, 2014

Makosa 7 yanayopelekea biashara nyingi kutofanikiwa.

Kuanzisha biashara kwa watu wengi ni changamoto ambayo hawawezi kuikabili. Kuanzisha biashara yako binafsi yaweza kukuletea faida kwa njia nyingi ikiwemo kujitambua zaidi, kupata uhuru za kifedha (financial independence), fursa ya kuweka alama (mark) katika maisha yako na pia kuwa katika nafasi ya kutoa mchango chanya katika jamii yako au sehemu ya kibiashara.

Katika kufikia hayo watu wengi hufikia kuanzisha biashara zenye mafanikio na nyingine bila mafanikio. Makala hii inakuletea sababu tano za kwanini biashara nyingi ndogo hushindwa kufanikiwa:-

1. Kutofanya Utafiti wa kimasoko

Biashara nyingi hushindwa kufanikiwa kwa sababu ya kutofanya utafiti wa kutosha wa kimasoko (market) ambayo hupelekea mfanyabiashara kuingia katika biashara yenye watu wafanyabiashara wengi tayari au biashara ambayo wateja hawapo na uelewa mzuri juu yake, eneo (location) ambayo sio sahihi. Hasara ambazo mtu anaweza pata kwa sababu ya kujiingiza katika biashara bila kufanya utafiti.
Bila utafiti mfanyabiashara anaweza kuanza kuuza vifaa vya kisasa kama simu, Tablets na computer katika kijiji kisicho na umeme au kuuza bidhaa maarufu kama adidas, Gucci na Macintosh kwa wateja wasio na TV. Biashara yako inatakiwa iangalie matatizo au watu wanachohitaji kutokana na mazingira yao.

2.  Nafasi ya kisheria ya biashara husika.

Kosa lingine ni Mara nyingi wajasiriamali huingia katika biashara bila kufuatilia sheria inasemaje juu ya biashara hiyo kwenye eneo analotaka kufanyia biashara, wanashindwa kufuatilia taratibu za utunzaji wa mazingira na upatikanaji wa ruhusa mfano biashara za kusafirisha mizigo, mkaa, na biashara ndogondogo katika maeneo ya mijini (mfano, Dar es Salaam).

Pia hapa tunazungumzia ulipaji wakodi au usajili wabiashara hiyo kupitia usajili wa biashara ambayo sio sahihi kulinganisha na kipato cha biashara hiyo. Mfanyabishara anatakiwa kufuatilia msamaha wa kodi na ajue ni usajili wa aina ipi waweza kumsaidia kwa kumtoza kodi halali na yenye unafuu kutokana na umri wa biashara yake na faida anayopata.
  
3.  Eneo (location) na kuwafikia wateja

Uamuzi wa uuze wapi bidhaa zako ni rahisi, inatakiwa iwe eneo amablo watu wataweza kukufikia kirahisi. Inatakiwa iwe located sehemu ambayo watu wana uhitaji wa hiyo bidhaa. Iwe mahala ambapo wewe kama mfanyabiashara waweza pata bidhaa unazouza au rasilimali za biashara yako kirahisi.

4.   Kushindwa kuanza kama biashara ndogo.

Ubora wa bidhaa ni kuwa sahihi kwa lengo husika. Sio lazima kuanza biashara kwa kununua flame au kununua duka ambalo ni Fixed Assets, watu wengi hujaribu kuanza kwa kuwa mobile mara nyingine si kwa kupenda lakini hii husaidia kutengeneza custumer base kabla hawajakuza biashara yake.
Biashara ndogo ndogo zinazoanza bila Fixed Assets zinanafasi kubwa ya kukua na kulitambua soko kuliko zile zinazoanza kwa fixed assets.

5. Kuwa na nidhamu ya kifedha (Financial discipline)

Kuwa mfanyabishara mkubwa unatakiwa kuwa na uelewa wa kujaza fomu na documents nyingi mbalimbali za kimahesabu lakini haimaanishi kwamba utakuwa na uelewa wa biashara yenyewe. Watu wanaweza kuanzisha biashara bila ya kuwa na uwezo wakujaza au kusoma balance sheet au business plan.

Uelewa kiasi wa vitu hivi ndio unaohitajika pale mfanyabiashara anapohitaji mkopo huhitajika kwenda kueleza ni jinsi gani ataweza kutunza kiasi cha faida atayopata kabla hajapata mkopo.

Wafanyabiashara wadogo wadogo hukosa mikopo kwa kutojua jinsi ya kufanya mahesabu madogo na kuwa na nidhamu katika uhifadhi wa pesa.

6. Kukosa Ushauri wa mtu mwenye uzoefu (Mentor support, Second Opinion)

Wafanyabishara wengi hukosa kujikosoa kwani kwa kuwa tupo katika nchi yenye watu masikini basi wafanya biashara huweka eneo lake la biashara au bidhaa zake juu ya wateja na kuwadhalau wateja. Mteja ni mfalme kwa hiyo mfanyabishara anatakiwa kujikosoa kwa kuwauliza baadhi ya wateja wake kwa njia tofauti za kukusanya maoni.

Kwa mtu kuamua kutumia pesa yake kwako yahitaji awe atambue unajali. Wafanyabishara wengi wanashindwa kujua kwamba wateja wanatambua kuwa kitendo cha wao kununua kwako wanachukua hatua ya kuwa-support na kudhani au kuwa-treat kana kwamba wateja hao hawana sehemu nyingine ya kwenda kujipatia mahitaji hayo.

7.  Teamwork and Networking

Katika ushindani ulipo sasa hivi ni vizuri mfanyabiashara kujiunga katika vikundi mbalimbali ili aweze kujitangaza pamoja na kuwajua wafanyabishara wenzake ambao wanaweza kumsaidia kwa mawazo na hata kwa wateja pale wanapoishiwa bidhaa Fulani katika maduka yao.

Haya ni makosa 7 ambayo wafanyabishara wadogo au wanaoanza huyafanya kwa kujua au bila kujua. Kwa kufuatilia BusinessTOK utapata kuwasikiliza wafanya biashara wataoweza kuongelea mada hii.


Usisite kuweka maoni yako juu ya makala hii hapa chini.
Back To Top
Don't You Think this Awesome Post should be shared ??
| Makosa 7 yanayopelekea biashara nyingi kutofanikiwa. |