Breaking News
Loading...

PHOTO OF THE DAY

STUDENTS CORNER

START UP LAB

Recent Post

Tuesday, November 29, 2016
Kituo Kipya

Kituo Kipya


Kwa nini vijana wa Kitanzania hawana uwezo wa kuziona fursa, wamezubaa sana, hawajui umuhimu wa kuwa wakwanza katika kufanya maamuzi. Leo hii wengi wa vijana wakianzania hawana utashi katika jambo lolote lile, wanazurula barabarani wakisubiri miujiza, leo ni siku ya tatu tangu nibandike tangazo hili la kuwasaidia na hakuna aliyenitafuta. Inamaana hata wazazi nao hawashughuliki kutafuta upenyo wa watoto wao, nao pia wanajidanganya kuwa muujiza wa mkopo utawatokea ama serikali italegeza masharti.

Mimi ninaanza darasa hata na watu wawili na sitafungua tena dirisha la kuandikisha. Wazazi wanakimbilia pre form one, kama walivyofanya miaka hiyo, hawana utashi wanatengeneza watoto wanofanana na wengine, hawajui dhana ya competition.  Hata unapotoa offer ya kutmia muda wako wazazi wamebaki vipofu, wanataka vitu vya bure, ukiwaambia unawaita kuwaona wasanii, wazazi watawapa watoto na hela ya soda, huu ndio umasikini mnaoujenga kwenye familia zenu. Watanzania wengi watabaki na umasikini kwa kuwa wanaupenda na kuuzoea.  Mpaka leo unangoja nini kumuandikisha mtoto wako kwenye kituo chetu? Tena wale wa tegeta wasio na uwezo wa hata nauli, wamelala wanangoja nafasi hizi zijazwe na wa mjini, mungu anisaidie nisiwe mmojawapo wa wazazi wapumbavu, maana watu hawa wameandikwa mpaka kwenye biblia, sawa na wale wanawali watano wapumbavu walioenda na taa zisizo na mafuta, mungu wasaidie wako


Thursday, October 20, 2016
no image

Register for the meeting to complete your Application for Australian Scholarships

Fill on this or Face to Face with Rosemary Mwakitwange Blog to book a space to participate in the assisted application filling meeting to be held on November 9, 2016 humu ama kwenye blog Face to Face with Rosemary Mwakitwange
Tuesday, March 8, 2016
no image

Bado vijana wa kitanzania hawajaamka kutafuta maisha,

Ni jambo la kushangaza sana kwamba vijana wa kitanzania wamekataa kuchukua hatua ya kubadilisha maisha yao. wanataka kazi lakini hawataki kabisa kujifunza nini cha kufanya ili kupata hizo kazi, Kazi ziko tele zinatangawa kila siku kwenye mitandao, waajiri wanatafuta watu wa kuwaajiria vijana wamekaa  nyumbani hawataki kujifunza. Nashukuru sana kwa wale wachache waliohudhuria kozi yetu pale Regency Park Hotel, mikocheni, ninaamini walijifunza kitu na wengine tunaendelea kuwasaidia katika ktuengeneza proposal zao za biashara, wengine wamehudhuria zile interview walizokuwa wanatarajia kwa kufanikiwa, wengine wameanza kuitwa kwenye usaili kwa kuwa hata barua zao za usaili wamebadilsha namna yakuziandikisha. Lakini wengine mamia bado mko huko vijiweni mnapiga domo na siku zinaekwenda.  Tukufanyie nini? Hakuna chochote under the sun utakachoweza kufanya kama huna skills zinazotakiwa, vijana wengi mmejaa uvivu na mnategemea miujiza, hata hiyo miujiza haiwezi kuwafuata vyumbani mliko. Tunaendelea na vipindi vya mafunzo chuoni kwetu maalumu kwa vijana waliomaliza form four na pengine hawakufanikiwa kupata grade za kuwapeleka form five, tunajua mko wengi sana na bado mmekaa majumbani, ninatamani hata wazazi wenu wangehusika na maisha yenu maana wakati wa kutengeneza ni huu, muda ukipita hutakua na nafasi tena, tuna nafasi 10 tunataka kuchukua vijana wa kuwafundisha project management kwa ktumia computer, masomo ni ya mwezi mmoja tu wa April, na malipo ni sh 100,000/- kwa huo mwezi. hakuna namna ya sisi kuwapatia masomo bure, kuna garama za uendeshaji, kama uko tayari kupata kitu tofauti mwezi huu tupigie simu na ufike kujiandikisha. idadi ya wanafunzi tunayochukua ni sawa na idadi ya computer tulizo nazo.

Natumaini dalili ziko wazi huko tunakokwenda hakuna tena ubabaishaji wa mtu kupata kazi yoyote kwa mjomba ama shangazi ama kwa jina la baba, serikali ya awamu ya tano iko serious na elimu, njoo walau upate pa kuanzia, tupo kwa ajil yako kama hutatutumia hasara ni yako


Back To Top